Saturday, January 14, 2012

Wasee hii story ya 2013 sijuwi 2015 kuna vile haileti bidii na imefanya ni kubuke Mashifta  na ngoma yao ya 'System ya majambazi' dem dayz. You see kama vile Mashifta walinena nafaa kuongeza kuwa "hii ngava pia ni ya majambazi"!! Cheki hii story ya election sasa. Tulikimbizwa ooh sijui na ndizi, mara chungwa then tunajistukia kuna vile tulikuwa tunaingizwa kwa fix jo. Sheria imekuwa kizungumkuti na hao mawakili na majaji pia nataka kuwaongeza kwa hiyo ngoma pia...majaji Majambazi!! Kulingana na vile koti iliamua kuna vile kuna solution mbili towards changing leadership in motherland but kuna vile ni kama huyo judge alicheki hiyo haiwezekani. Story ni hii, Kama Rao na Ubakz wanaweza nego na wavuje hiyo coalition kuna vile tunaweza enda kwa Dembe in Aug ama Dec. Najuwa labda watu wengi wanauliza wassup na ma election na wanasiasa ni walewale, cheki mseehii gava ya coalition kuna vile imeruin storo mob. Actually hio miaka tano nacheki ni kama imekatika hivyo jo. You see coalition haikucome kutusort, iliundwa tu coz ya zile nuksi za 2007. Cabinet ikafanywa kuwa bwaku ili hao ma tumbo kubwa wapate vyeo. Hiyo design haikuwa poa but kuna vile kilikuwa kimetee in 2007 so hata nyundo wa komeo hangeweza kuunda any. Sasa ni poa tupate ma leaders wapya jo coz sisi mavijanaa kuna vile tumeteseka sana. Tulizaliwa tukishoiwa sisi ni ma leaders wa moro then sasa tushazeeka na moro haifikangi. Cheki mavijanaa hawana works, actually na shindwa tukizeeka tutakuwa generation gani jo? Wasee wa mine wao hujiita generation sumbua, but tunasuffer na hatujafanya kitu. Hao mabunda kuna vile wametuwaste na  ndio tunataka dere mwingine na hakuna story na koda tena.
Kenya ni yetu sote, ma grandi walipigania uhuru [RIP] ili sisi tukae poa but mpaka waleo hatujawahi kaa poa. Hii ndio tym tunataka sasa kuona ni nani mkenya mzalendo sasa. Hao ma leaders wakikatalia hapo kuna vile sifa zao hazitakuwa poa, cmon miezi tatu after all itasaidia nini, mshahara?? Emilio tushampatia miaka kumi although hii ya mwisho kunavile nasikia alicheza kalongo. Sasa si ni poa atosheke na hiyo ashu jameni? Extension ya miezi tano tena ni ya nini baba.  Rao pia kuna vile namuona kwa hii mbio asha piga tizi na yuko tayari kuchomoka na medali. Sasa itakuwa aje kama unataka kuwin race ilihali bado unataka kufaidika na miezi tatu? Itakuwa intresting sana kucheki ni nani Mkenya mzalendo kati ya Rao na Emilio. Na mimi na uliza, Ni nani??